RAIS wa
Atletico Madrid, Enrique Cerezo amedai kuwa hakuna nafasi kwa mshambuliaji wao
Antoine Griezmann kujiunga na Real Madrid au Manchester United.
Nyota huyo
wa kimataifa wa Ufaransa jina lake limehusishwa na vilabu kadhaa vikubwa barani
Ulaya katika miezi ya karibuni kufuatia kuimarika kwa kiwango chake.
Tetesi za
kuhamia Old Trafford nazo zilizuka huku Griezmann akikiri kuwa angefurahi
kucheza sambamba na Mfaransa mwezake Paul Pogba huku Madrid nao wakitajwa
katika mbio za kumuwania.
Hata hivyo,
tetesi hizo zimezimwa na Cerezo akidai kuwa haamini kama mshambuliaji huyo
mwenye umri wa miaka 25 ataweza kwenda Madrid au klabu nyingine yeyote ile.
Cerezo aliendelea
kudai kuwa wamekuwa na uhusiano mzuri na Madrid na wanaheshimiana kama
majirani.
Atletico wanatarajiwa kuikaribisha Madrid
katika mchezo wa La Liga kesho, ikiwa ni mara ya kwanza kwa timu hizo kukutana
toka Atletico walipofungwa katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa matuta
Mei mwaka huu kule San Siro.
No comments:
Post a Comment