NA ANAEL JAMES WAZIRITALL
Umoja wa waganga wa tiba asiliaa (UWAWATA) wamesisitiza kwa wanachama
kukamilisha michango yao waliyo ahidi katika kituo cha kulea watu wenye ulemavu
wa ngozi Albino.
Hayo yamesemwa katika kikao mbele ya mratibu wa mratibu wa
chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi mkoa wa shinyanga bwn LAZARO ANAEL wakati akiongea na waganga hao na
kuomba kuaminika kuwa sio waganga wote
wanahusika na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yaani Albino na kusisitiza kusakwa kwa
waganga wanaopiga ramli chonganishi.
Lakini mbali na hapo Mratibu wa chama cha watu wenye ulemavu
wa ngozi mkoa wa shinyanga wakati akiongea na mimi katika kikao hicho aliweza kuwaelimisha waganga wa tiba asilia juu ya
watu wenye ualbino na kusema kuwa wote wapo sawa na inatakiwa kuondoa matabaka
yaliyopo ili uwepo usawa na pia waweze kusaidia jamii katika kupinga waganga
wapiga kamli chonganishi ili na wao waweze kuishi kwa kuwa wana haki ya kuishi
Lakini pia Katibu wa nidhamu kanda ya ziwa na mjumbe wa
kamati ya nidhamu kitaifa BWN DAVID SIMLEMBE amewataka waganga wa tiba asili
kujitambua kwa mambo wanayoyafanya na pia
kutimiza ahadi waliyo ahidi katika kituo cha watu wenye ulemavu wa ngozi
albino na kuwaomba waganga wote kukutana katika kikao cha jumamosi ili
kuzungumzia mambo mengi yanayowakabili.
No comments:
Post a Comment