Na Anael James Waziri_Tall
Ni kauli ya Staa huyo wa Wekundu wa msimbazi Wakati zikiwa zimebaki siku nne pekee kabla ya mechi ya watani Simba na Yanga kupigwa, mshambuliaji wa huyo, Mrundi, Laudit Mavugo, ameweka bayana yeye haongei sana kuhusu mchezo huo utakavyokuwa, lakini anasubiri tu siku ifike ili aonyeshe makali yake uwanjani.
Ni kauli ya Staa huyo wa Wekundu wa msimbazi Wakati zikiwa zimebaki siku nne pekee kabla ya mechi ya watani Simba na Yanga kupigwa, mshambuliaji wa huyo, Mrundi, Laudit Mavugo, ameweka bayana yeye haongei sana kuhusu mchezo huo utakavyokuwa, lakini anasubiri tu siku ifike ili aonyeshe makali yake uwanjani.
Mshambuliaji huyo aliyeifungia Simba mabao matatu mpaka sasa, kwa mara ya kwanza
anatarajia kuiongoza timu yake hiyo kuvaana na Yanga katika mchezo huo
utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Oktoba Mosi, mwaka huu.
Mshambuliaji
huyo wa zamani wa Vital’O ya Burundi, amesema licha ya presha ya mchezo
huo inavyozidi kupanda lakini kwa upande wake hataki kuzungumzia lolote
kuhusiana na wapinzani wao, bali atawaonyesha watakapokutana uwanjani.
“Mechi
itakavyokuwa vyovyote kwangu sawa kwa sababu nipo tayari na nimejiandaa
kucheza na sina wasiwasi ila kwa wale ambao watataka kuona nitafanya
nini basi waje kuona uwanjani na siyo kuanza kuongea sana kabla mechi
yenyewe haijachezwa,” alisema mshambuliaji huyo wa Wekundu wa msimbazi
.
No comments:
Post a Comment