Na Anael James Waziri_Tall
Baada
ya kuchezea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa wapiga debe wa Stendi ya Shinyanga,
Stand United Chama la wana, Kikosi cha Yanga kinatarajia kuendelea kuweka kambi kanda ya ziwa, kwa ajili ya kujiandaa
na mechi yake dhidi ya watani wao wa jadi, Simba itakayochezwa Jumamosi
ijayo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit, alisema kikosi chao kinatarajia kuendelea kuweka kambi katika kanda ya ziwa kabla ya kurejea kwa ajili ya kuwakabili wekundu wa msimbazi Simba Oktoba Mosi.
“Kikosi
chetu kitaendelea kuweka kambi katika kanda ya ziwa
kwa ajili ya kujiandaa na mechi yetu dhidi ya Simba ambapo tutarejea
siku chache kabla ya mchezo huo.
“Mchezo dhidi ya
Simba ni wa kawaida kwetu na tunajiandaa kama ilivyo kwa mechi
nyingine kwani tumeshakutana na timu kubwa na kuonyesha uwezo mkubwa Zaidi, hivyo
tunaupa uzito sawa mchezo huo na ile mingine na kikubwa Zaidi mwalimu hajatoa ripoti ya mchezaji yoyote aliye majeruhi,” alisema katibu huyo wa wana Jangwani Baraka.
No comments:
Post a Comment