NDUGU WA OBAMA KUWA MGENI WA DONALD TRUMP KWENYE MDAHALO - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Thursday, October 20

NDUGU WA OBAMA KUWA MGENI WA DONALD TRUMP KWENYE MDAHALO

NA ANAEL JAMES WAZIRI_TALL
Maafisa wa kampeni wa mgombea urais wa chama cha Republican Donald Trump wamepanga kumwalika kaka wa kambo wa Rais Barack Obama kuhudhuria mdahalo wa mwisho wa urais nchini Marekani.
Maafisa hao wamesema Malik Obama, ambaye alizaliwa Kenya, atakuwa miongozi mwa hadhira itakayofuatilia mdahalo huo wa runinga, Bw Trump alikabiliana na mpinzani wake wa chama cha Democratic Hillary Clinton.
Malik, aliambia gazeti la New York Post kwamba ana furaha isiyo na kifani kwamba atahudhuria mdahalo huo.
"Trump anaweza kuirejeshea Marekani fahari yake tena," amesema, kwa mujibu wa shirika la habari la AP.
Wagombea wamekuwa wakitumia wageni kwenye midahalo kama njia ya kuwakabili wapinzani wao.

Source:BBC

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here