ARSENAL YAPATA PIGO KUBWA:SOMA HAPA - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Wednesday, November 9

ARSENAL YAPATA PIGO KUBWA:SOMA HAPA

NA ANAEL JAMES WAZIRI_TALL

Klabu ya Arsenal iko kwenye wasiwasi mkubwa ikisubiri kujua hali ya Fowadi wao Alexis Sanchez ambae ameumia Musuli za Mguuni akiwa Mazoezini na Timu ya Taifa ya Nchi yake Chile.

Alex's Sanchez

 Chama cha Soka cha Chile kimetoa Taarifa kuthibitisha kuumia kwa Sanchez na kusema Mchezaji huyo atabaki Santiago, Chile wakati Timu inasafiri kwenda kucheza na Colombia Alhamisi Usiku kwenye Mechi ya Kanda ya Nchi za Marekani ya Kusini kuwania kufuzu kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 huko Russia.
 
Kisha Chile itarejea kwao kucheza na Uruguay hapo Jumanne Novemba 15.
Sanchez, mwenye Miaka 27, Msimu huu ameifungia Arsenal Bao 8 na ikiwa atakaa nje kwa muda mrefu ni pigo kubwa kwa Timu yake.
 
Mechi inayofuata kwa Arsenal baada ya Wiki hizi 2 za Mechi za Kimataifa ni dhidi ya Manchester United huko Old Trafford hapo Jumamosi Novemba 19 ikiwa ni Mechi ya EPL, Ligi Kuu England, na kisha ni ile ya UEFA CHAMPIONZ LIGI Jumatano Novemba 23 dhidi ya Paris Saint-Germain Mechi ambayo ni muhimu kuamua nani ataibuka Mshindi Kundi A.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here