Wekundu wa msimbazi wamemaliza mkutano wao kwa amani na Katika mkutano huo ulioongozwa na Rais wa klabu, Evans Elieza Aveva na kuhudhuriwa na wanachama 642 kati ya zaidi 5,000 wa klabu hiyo – mabadiliko ya Katiba yalipita kwa kishindo.
Wanachama
wengi waliunga mkono kwa utulivu muda wote wa mkutano kufuatilia kwa
makini kipengele kimoja hadi kingine kati ya vilivyojadiliwa.
Kipengele hicho cha uendeshwa wa klabu kwa hisa kitawekwa katika ibara ya 49 ya klabu ya Simba.Vipengele vingine vyote vidogo vilivyomo ndani ya Ibara hiyo vilipitishwa pia kama cha 49 (i) kinachosomeka; Uamuzi wowote wa kubadilisha mfumo, kuvunja au kufutwa kwa Simba unahitaji theluthi ya 2/3 za wanachama wote wa Simba waliopatikana katika mkutano mkuu uliopitishwa maalum kwa madhumuni hayo. Kipengele cha 49 (ii) kinasomeka; Hakutakuwa na mabadiliko na kipengele cha 49(iii) kinasomeka; Kuwepo na sababu za kubadilisha mfumo, kuvunja au kufutwa kwa Simba kama vile kuwa na madeni makubwa yasiyolipika, kupoteza hadhi ya kutoaminika na kukopesheka au kuendana na matakwa ya mfumo wa nyakati za biashara.
Katika
ibara 49 (a) kipengele kilichopitishwa kinasema mkutano wa wanachama
unaweza kuitishwa kwa mujibu wa Ibara ya 22 na kufanya mabadiliko ya
mfumo wa umiliki au uendeshwaji wa Simba.
Kwa
upande wa kipengele (b) chenyewe kinasema mabadiliko ya mfumo wa
uendeshwaji au umiliki wa Simba hayataathiri hadhi ya wanachama wote
halali wa Simba isipokuwa hadhi hiyo itabadilika kuendana na mfumo
stahiki wa mabadiliko yaliyofanyika.
Uwiano
wa thamani ya umiliki wa kila mwanachama katika mfumo mpya utajadiliwa
na Kamati ya Utendaji kutokana na thamani ya klabu na uwekezaji.
Kipengele
(c) cha ibara hiyo kinaeleza kuwa mfumo mpya wa mabadiliko ya
uendeshaji au umiliki wa Simba utarithi haki na mali zote pamoja na
madeni na wajibu wowote uliokuwa chini ya Simba kabla ya mabadiliko
hayo.
Kipengele
(d) na cha mwisho cha Ibara hiyo kinasema mabadiliko ya mfumo wa
umiliki au uendeshaji wa Simba yatabainisha kuacha kutumika kwa katiba
hii na mkutano mkuu chini ya mfumo mpya utapitisha katiba mpya chini ya
utaratibu wa haki na kura za mfumo huo mpya.
Baada
ya wanachama kupitisha kipengele hicho, Rais Aveva aliwataka kuwa
watulivu wakati huu ambao mabadiliko hayo yatapelekwa Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo na mwisho
kwa Msajili wa Vyama na Klabu za Michezo ili yapitishwe na kuwa Katiba
kamili.
Mkutano
huo unafuatia mwanachama wa Simba na mfanyabiasha maarufu nchini
Mohamed ‘Mo’ Dewji kutoa ofa ya kununua asilimia 51 ya hisa za klabu
hiyo kwa Sh. Bilioni 20.
Hata
hivyo, Baraza la Wadhamini la klabu, chini ya Mwenyekiti wake, Hamisi
Kilomoni lilipinga Mkutano huo likitaka kwanza wanachama wahakikiwe na
Baraza la Michezo. Hakukuwa na kiongozi wa BMT wala Serikali kwa ujumla
kwenye mkuatano huo.
No comments:
Post a Comment