Kiungo Ibrahim Ajibu sasa ana hadi nafasi ya asilimia 70 kupata nafasi ya kuitumikia Haras El Hodood ya Misri.
Ajibu amepasi vipimo vya afya, maana yake nafasi ya kukipiga nchini Misri ni kubwa kama ambavyo taarifa zimeeleza.
Amepewa muda wa wiki moja na nusu wa majaribio na unaisha Desemba 31.
Abdel
Haidar anayejishughulisha na masuala ya afya katika timu hiyo ya Jeshi
la Misri, amezungumza na Championi kutoka Alexandria Misri na kusema
hiyo ni hatua kubwa kwa Ajibu.
“Amefuzu vipimo vya afya. Hii ni hatua kubwa zaidi, sasa yamebaki masuala baadhi ambayo yanamhusu kocha.
“Kocha sasa anaendelea naye na mwisho atatoa maelezo kuhusiana na suala la vipimo vya afya,” alisema Haidar.
Wakati
Haidar anasema hivyo, Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Usajili ya Simba,
Kassim Dewji amesema wanasubiri kuhusiana na Ajibu hadi Desemaba 31.
“Taarifa
za maendeleo yake tunazifuatilia kwa karibu kabisa. Tunajua hilo la
vipimo vya afya lakini sisi hatutalizungumzia kwa kuwa anaendelea na
majaribio hadi Desemba 31.
“Baada
ya hapo, tunaamini timu hiyo itaanza mawasiliano nasi. Hivyo nafikiri
mgevuta subira,” alisema Dewji maarufu mama Gwiji ambaye amewahi kuwa
katibu mwenezi wa kikosi cha Simba kilichotinga fainali ya Caf mwaka
1993 na katibu mkuu wakati Simba ikiing’oa Zamalek Klabu Bingwa Afrika
mwaka 2003.
Kama Ajibu atakuwa amefuzu vipimo vya afya maana yake ni sawa na kufuzu kuichezea timu hiyo kwa asilimia 80.
Hata
hivyo, kama atafuzu na kujiunga nayo atakuwa na kazi ngumu kuhakikisha
anapambana kuisaidia kurejea Ligi Kuu Misri baada ya kuwa imeshuka msimu
uliopita.
Kwa Tanzania, Haras El Hood kwa kile kipigo cha mabao 5-1 ilichokitoa kwa Simba katika michuano ya Ligi ya Mabingwa.
No comments:
Post a Comment