Ikiwa ni mechi ya kwanza kwa mwalimu wa Yanga SC George Lwandamina ni BAO 2 za Emmanuel Martin za mapema Kipindi cha Kwanza zimewapa JKU ya Zanzibar ushindi wa 2-0 walipocheza na Mabingwa wa Tanzania Bara Yanga Mechi ya Kirafiki Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kwenye Mechi ya kwanza kabisa chini ya Kocha kutoka Zambia George Lwandamina.
Lwandamina, aliechukua wadhifa huo Wiki 2 zilizopita kutoka kwa Mholanzi Hans van der Pluijm ambae amekuwa Mkurugenzi wa Ufundi hapo hapo Yanga, Leo alikuwa akisimamia Mechi yake ya kwanza na hilo lilionekana kwenye upangaji wa Timu kwani alijaribu kumpa nafasi kila Mchezaji.
Mzambia huyo, Kipindi cha Pili, alibadili Wachezaji 10 kwa kuwaingiza Deogratius Munishi 'Dida', Juma Abdul, Mwinyi Hajji Mngwali, Vincent Bossou, Justin Zulu, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Simon Msuva, Amissi Tambwe na Deus Kaseke.
Licha ya kosa kosa kadhaa, Mabadiliko hayo hayakuwapa Yanga Boa lolote.
Jumamosi ijayo Yanga watakuwa hapo hapo Uhuru
No comments:
Post a Comment