Rais Mugabe aanza kampeni za uchuguzi mkuu wa mwaka 2018 - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Saturday, June 3

Rais Mugabe aanza kampeni za uchuguzi mkuu wa mwaka 2018


Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe aanza kampeni za uchaguzi mkuu nchini unaotarajiwa kufanyika ifikapo mwaka 2018.

Rais Mugabe ameanza kampeni hizo akionekana kuwavutia vijana.

Hapo Ijumaa rais Mugabe alianza kampeni zake kwa kutembelea eneo la Marondea , eneo ambalo linapatikana katika umbali wa kilomita 80 na jiji la Harare.

Katika eneo hilo rais Mugabe alifanya kampeni katika uwanja wa Rudhaka .

Licha ya kutuhumiwa kudhoofisha sekta ya kilimo baada ya kuwanyanganya wakuliwa wa kizungu mashamba, rais Mugabe amesema kuwa uchumi wa Zimbabwe unafanyiwa njama na Magharibi.

Rais Mugabe aliendelea kusema kuwa Zimbabwe sio taafa maskini na kuahidi kuwa katika sekta ya kilimo mavuno yataongezeka katika zoa la mahindi na tumbaku.

Mugabe atakuwa atakuwa mgombea wa kiti cha urais kupitia chama ZANU –PF katika uchaguzi unaotarajiwa katikati mwaka 2018.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here