Ajali yaua watu 13 Uganda - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Monday, September 18

Ajali yaua watu 13 Uganda



Watu 13 wamepoteza maisha na wengine kadhaa wamejeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea Katonga wilayani Mpiji nchini Uganda.

Ofisa wa polisi wa Katonga, Philip Mukasa amesema ajali hiyo imetokea usiku wa kuamkia leo Jumatatu ikihusisha basi aina ya Toyota  Coaster lililogongwa na lori.

Mukasa amesema basi lililohusika katika ajali hiyo lina namba ya usajili ya Tanzania na lori lina namba za Uganda.

Amesema lori lililokuwa katika mwendokasi lilipasuka gurudumu hivyo kuyumba na kugonga gari hilo la abiria.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here