Na Anael James Waziri_Tall
MENEJA wa Real Madrid, Zinedine Zidane amekataa kukipa
nafasi kikosi chake wakati wakijiandaa kutetea taji lao la Ligi ya Mabingwa
Ulaya kwa kucheza Sporting Lisbon leo usiku.
Ushindi wa changamoto ya mikwaju ya penati dhidi ya mahasimu
wao wa jiji Atletico Madrid, uliwapa vijana hao wa Santiago Bernabeu taji la 11
la michuano hiyo Mei mwaka huu.
Akihojiwa kama anadhani kikosi chao kinaweza kutetea taji
hilo msimu huu, Zidane amesema suala hilo linaweza kuwa gumu kwani kuna timu
nyingi zinazoweza kushinda hivyo inabidi wapambane.
Meneja huyo aliendelea kudai kuwa jambo muhimu ni
kuhakikisha wanajiimarisha na kushinda kila hatua ili waweze kufikia malengo
yao.
No comments:
Post a Comment