Na Anael James
MANCHESTER UNITED Leo wanatinga Uwanjani kwao Old Trafford kucheza Mechi yao ya 5 ya Kundi A la UEFA EUROPA LIGI wakisaka ushindi ili kujiweka hai kwenye 2 Bora ambazo zitaingia Raundi ya Mtoano ya Timu 32.
Hii ni moja ya Mechi zote za 5 za Makundi zinazochezwa Leo na baada ya hii kila Timu itabakiza Mechi 1 tu itakayochezwa Desemba 8.
Kwenye Kundi A, Man United wapo Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 1 nyuma ya Vinara Fenerbahce wenye Pointi 7 kama vile Feyenoord.
Man United, ambao wameshinda Mechi zao zote 2 za Kundi A walizocheza Old Trafford na Fenerbahçe na Zorya Luhansk, Leo wanacheza na Feyenoord ambayo, bila kutegemewa, iliifunga Man United 1-0 huko Rotterdam Mwezi Septemba kwenye Mechi ambayo Man United na walistahili kushinda.
Meneja wa Feyenoord, Giovanni van Bronckhorst, Mchezaji wa zamani wa Arsenal, anaihofia Man United akitegemea kusulubiwa na hata fomu ya Timu yake sio nzuri kama mwanzoni mwa Msimu waliposhinda Mechi zao 11 za kwanza kati ya 12, moja ikiwa dhidi ya Man United.
Lakini hivi karibuni wameshinda Mechi 1 tu kati ya 5 ingawa Wikiendi iliyopita waliipiga 3-0 PEC Zwolle kwenye Ligi ya kwao Holland.
Wakati Feyenoord itawakosa Terence Kongolo na Eric Botteghin kutokana na Majeruhi na kufungiwa, Man United Majeruhi wao ni Eric Bailly na Chris Smalling wakati ipo hatihati kwa Marouane Fellaini kucheza kutokana na Musuli za Mguu kumsumbua.
Meneja wa Man United, Jose Mourinho, anatarajiwa kubadili Kikosi toka kile kilichotoka 1-1 na Arsenal na mmoja wa Wachezaji ambao watacheza hii Leo ni Henrikh Mkhitaryan ambae amekuwa hachezeshwi na pia Zlatan Ibrahimovic alieikosa Mechi na Arsenal kwa kuwa Kifungoni.
VIKOSI:
Man United: De Gea – Valencia, Jones, Bailey, Rojo – Pogba, Herera – Mata, Rooney, Mkhitaryan – Ibrahimovic
Feyenoord: Jones – Van der Heijden, Nelom, Botteghin, Karsdorp – El Ahmadi, Kujit, Vilhena – Elia, Jorgensen, Toornstra
REFA: Manuel Gräfe (Germany)
RATIBA YA GAME NYINGINE
KUNDI A
19;00 Fenerbahçe v Zorya Luhansk
23;05 Manchester United v Feyenoord
KUNDI B
19;00 FC Astana v Apoel Nicosia
23;05 Olympiakos v BSC Young Boys
KUNDI C
1900 FK Qabala v RSC Anderlecht
2305 Saint-Étienne v Mainz 05
KUNDI D
1900 Zenit St Petersburg v Maccabi Tel-Aviv
2305 Dundalk v AZ Alkmaar
KUNDI E
23;05 Austria Vienna v Astra Giurgiu
23;05 Roma v Viktoria Plzen
KUNDI F
23;05 Athletic Bilbao v Sassuolo
23;05 KRC Genk v Rapid Vienna
KUNDI G
21;00 Ajax v Panathinaikos
21;00 Celta Vigo v Standard Liege
KUNDI H
21;00 KAA Gent v Sporting Braga
21;00 Shaktar Donetsk v Konyaspor
KUNDI I
21;00 FC Schalke 04 v Nice
21;00 FK Krasnodar v FC Red Bull Salzburg
KUNDI J
21;00 Fiorentina v PAOK Salonika
21;00 Slovan Liberec v FK Qarabag
KUNDI K
21;00 Hapoel Be'er Sheva v Inter Milan
21;00 Sparta Prague v Southampton
KUNDI L
21;00 FC Zürich v Villarreal
21;00 Steaua Bucharest v Osmanlispor
No comments:
Post a Comment