Na Mustafa Ismail
Chapisho la kibaguzi kuhusu mke wa rais wa Marekani Michelle Obama limezua utata unaomuhusu meya wa jimbo la Virginia.
Pamela
Ramsey Taylor ,ambaye anaendesha shirika moja la kihisani katika kaunti
ya Clay, alimfananisha Michelle Obama na 'sokwe' .'Itakuwa vyema kuwa na mtu anayefuata mitindo,mrembo na mke wa kwanza mwenye heshima.Nimechoka kuona sokwe lililovaa viatu'',alisema.
Meya mwengine kutoka eneo hilo Beverly Whaling alijibu kwa kusema ''umeifanya siku yangu nzuri''.
Katika kaunti ya Clay zaidi ya asilimia 98 ya wakaazi 9,000 ni watu weupe.
Licha ya idadi hiyo ndogo katika jimbo hilo ,chapisho hilo la facebook lilisambaa nchini Marekani na katika vyombo vya habari vya kimataifa huku ombi la kuwataka wanawake wote wawili kufutwa kazi likikusanya saini 85,000.
Gazeti la The Washington post na lile la New York Daily yaliripoti kwamba bi Taylor aliondolewa katika wadhfa wake siku ya Jumatatu.
No comments:
Post a Comment