KUELEKEA SIKU YA TUZO YA MWANASOKA BORA WA DUNIA,HAYA NDIYO MAJINA YALIPITISHWA LEO NA FIFA - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Saturday, December 3

KUELEKEA SIKU YA TUZO YA MWANASOKA BORA WA DUNIA,HAYA NDIYO MAJINA YALIPITISHWA LEO NA FIFA

                       Image result for fifa 
FIFA imetangaza Wagombea Watatu wa mwisho kutoka Listi ya Wachezaji 23 wa kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani kwa Mwaka 2016.
 
Watatu hao ni Cristiano Ronaldo (Portugal/Real Madrid), Antoine Griezmann (France/Atletico Madrid) na Lionel Messi (Argentina/FC Barcelona). 

Kwa upande wa Kinamama, Wagombea ni Melanie Behringer (Germany/FC Bayern Munich), Carli Lloyd (USA/Houston Dash) na Marta (Brazil/FC Rosengård).

Kwa upande wa Makocha, Wagombea wa mwisho pia wametajwa na kwa Wanaume ni Claudio Ranieri (Italy/Leicester City), Fernando Santos (Portugal/Timu ya Taifa ya Portugal) na Zinedine Zidane (France/Real Madrid)

Kwa apande wa Kinamama Wagombea ni Jill Ellis (USA/Timu ya Taifa ya USA), Silvia Neid (Germany/Timu ya Taifa ya Germany) na Pia Sundhage (Sweden/Timu ya Taifa ya Sweden).

KURA KUPATA WASHINDI:
-Washindi wa Tuzo hizi watapatikana kwa Kura:
-Asilimia 50 ni ile ya Makepteni na Makocha wa Timu za Taifa za Nchi Wanachama FIFA
-Asilimia 25 ya Kura itatoka kwa Kura za Mtandaoni za Mashabiki
-Asilimia 25 ni Kura za Wawakilishi 200 wa Wanahabari kutoka Mabara yote 6 Duniani.

Vilevile Wagombea Watatu wa Goli Bora la Mwaka wametangazwa kutoka 10 wa awali na hao ni Marlone (Brazil/Corinthians), Daniuska Rodriguez (Venezuela/Venezuela Timu ya Taifa ya Wanawake U-17) na Mohd Faiz Subri (Malaysia/Penang).
Washindi wa Tuzo hizo za Ubora watatangazwa rasmi Januari kwenye Hafla maalum ya FIFA.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here