LEO BARCELONA KUCHEZA BILA MSAADA WA MSN,HABARI ZOTE HAPA - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Wednesday, December 21

LEO BARCELONA KUCHEZA BILA MSAADA WA MSN,HABARI ZOTE HAPA

Image result for MESSI
MABINGWA wa Spain FC Barcelona Leo watatinga Uwanjani kwao Nou Camp kucheza Mechi yao ya mwisho kwa Mwaka 2016 bila ya Nyota wao Watatu, maarufu kama MSN, ambao wamepewa Likizo ya Mapema.

Baada ya Mechi hizi za Leo Soka la Spain linakwenda mapumziko ya Krismas na Mwaka Mpya na kurejea baada ya Wiki ya Kwanza ya Januari.

Lakini Kocha wa Barca Luis Enrique ameamua Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar, ambao ndio hao MSN, pamoja na Gerrard Pique hawahitajiki kwa Mechi yao ya Leo na kuwaruhusu kwenda tangu walipomaliza Mechi yao ya Wikiendi walipoinyuka Espanyol 4-1.

Leo Barca wanarudiana na Timu ya Daraja la chini Hercules CF katika Mechi ya Pili ya Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ya Copa del Rey ambalo ni Kombe la Mfalme wa Spain.

Katika Mechi ya kwanza Timu hizi zilitoka 1-1.
COPA DEL REY
Raundi ya Mtoano ya Timu 32 - Mechi za Marudiano
Ratiba
o
(Kwenye Mabano Matokeo Mechi ya Kwanza)
21:00Sevilla FC v Formentera (5:1) 
21:00SD Eibar v Sporting Gijon (2:1)
23:00Osasuna v Granada CF (0:1)
23:00Valencia C.F v CD Leganes (3:1) 
23:00Deportivo La Coruna v Real Betis (0:1)   0:00FC Barcelona v Hercules CF (1-1)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here