Baada ya miaka 11, hatimaye Klabu ya Manchester United imerudi kileleni mwa listi ya vilabu tajiri duniani. United imepata mapato makubwa kuliko timu yoyote katika msimu uliopita kulingana na taarifa zilizochapishwa na kampuni kubwa ya ukaguzi duniani (Deloitte).
Manchester United imewashinda Real Madrid waliofanya vizuri katika michezo kwa miaka 11 baaada ya kukusanya mapato makubwa ya takribani Euro 689 katika msimu wa 2015-2016.
Ukijumlisha vipato vya timu ishirini bora kwa msimu wa 2015-2016 vimeongezeka kwa asilimia 12% na kufikia euro billioni 7.4 hii haijawahi kutokea.
Hii ni mara ya kwanza kwa Man U kushikilia nafasi hiyo tokea msimu wa 2003-04.
Real Madrid wameshuka mpaka nafasi ya tatu wakiwaacha wapinzani wao wakubwa Barcelona katika nafasi ya pili.
Mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich wapo nafasi ya nne huku matajiri wa jiji la Manchester Man City wakiwa nafasi ya tano kwa kutengeneza Euro milioni524 kwa msimu uliopita.
Hii ni mara ya kwanza kwa Man City kuingia katika 5 bora.
Listi kamili ya Delloite Money League ipo hivi.
Teams (positions last season) | Revenue in €m (£m in brackets) 2015-16 | Revenue 2014-15 |
1 (3) Manchester United | 689 (515.3) | 519.5 (395.2) |
2 (2) Barcelona | 620.2 (463.8) | 560.8 (426.6) |
3 (1) Real Madrid | 620.1 (463.8) | 577 (439) |
4 (5) Bayern Munich | 592 (442.7) | 474 (360.6) |
5 (6) Manchester City | 524.9 (392.6) | 463.5 (352.6) |
6 (4) Paris St-Germain | 520.9 (389.6) | 480.8 (365.8) |
7 (7) Arsenal | 468.5 (350.4) | 435.5 (331.3) |
8 (8) Chelsea | 447.4 (334.6) | 420 (319.5) |
9 (9) Liverpool | 403.8 (302) | 391.8 (298.1) |
10 (10) Juventus | 341.1 (255.1) | 323.9 (246.4) |
No comments:
Post a Comment