PAYET AIGOMEA WEST HAM ATAKA KUTIMKA,SOMA HAPA ZAIDI - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Thursday, January 12

PAYET AIGOMEA WEST HAM ATAKA KUTIMKA,SOMA HAPA ZAIDI

Image result for DIMITRI PAYET
MFARANSA Dimitri Payet ameiambia Klabu yake West Ham kwamba anataka kuondoka Januari hii kwa mujibu wa habari alizotoboa Meneja wa Klabu hiyo Slaven Bilic.
 
Akiongea na Wanahabari hii Leo kuelekea Mechi yao ya EPL, Ligi Kuu England, Jumamosi na Crystal Palace, Bilic amesema Mchezaji huyo amegoma kucheza Mechi hiyo ya Jumamosi.

 
Lakini Bilic amesisitiza licha ya Mchezaji huyo alienunuliwa na West Ham Mwaka 2015 kutoka Marseille kwa Pauni Milioni 10 kukataa kucheza, Klabu yao haina nia kumuuza.

Bilic amepasua kuwa Payet, mwenye Miaka 29, amesimamishwa kujiunga na Mazoezi ya Timu hadi sakata lake liishe.
Bilic amesema: “Hatumuuzi. Tumempa kila kitu lakini ametuangusha. Nimekasirika sana!”

Zipo ripoti kuwa Mchezaji huyo, ambae Februari Mwaka Jana alipewa Mkataba Mpya wa Miaka 5 na Nusu, anatakiwa huko kwao France huku Klabu za Marseille na Paris Saint-Germain zikitajwa sana.

Bilic mwenyewe amekiri kuwa anajua Payet amesharubuniwa na Klabu nyingine lakini yeye hajakata tamaa kubaki kwa Mchezaji huyo hapo West Ham.

Bilic amesema: “Natarajia atarudi na kuonyesha ari kwa Timu kama vile Timu ilivyomwonyesha yeye. Nimeongea na Klabu, Mwenyekiti na Makamu wake. Si suala la Fedha. Tunataka abaki!”

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here