RUFAA YA RAIS WA ZAMANI WA FIFA,SEPP BLATTER YAKATALIWA AKUBALI KIFUNGO,ZAIDI SOMA HAPA - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Monday, December 5

RUFAA YA RAIS WA ZAMANI WA FIFA,SEPP BLATTER YAKATALIWA AKUBALI KIFUNGO,ZAIDI SOMA HAPA

Image result for sepp blatter
MAHAKAMA ya Michzo ya Kimataifa-CAS, imetupilia mbali rufani ya rais wa zamani wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Sepp Blatter aliyepinga kufungiwa kujishughulisha na shughuli za soka kwa miaka sita. 

Blatter mwenye umri wa miaka 80, alifungiwa kufuatia kukiuka maadili ya shirikisho hilo aliloliongoza kwa miaka 17, kufuatia kashfa za ufisadi zilizoibuka mwaka jana.

 Blatter alikutwa na hatia ya kufanya malipo yasiyo halali ya paundi milioni 1.3 kwenda kwa rais wa zamani wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA Michel Platini ambapo wote walikanusha kufanya jambo lolote baya. 

Mara baada ya uamuzi huo wa CAS, Blatter amesema hatakata rufani na amekubaliana na uamuzi huo. 

Blatter aliongeza kuwa kwa uzoefu wake wa miaka 41 katika soka kikubwa alichojifunza ni kwamba unaweza kushinda katika mechi lakini pia unaweza kushindwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here