Maelfu ya panya wamevamia vijiji kadhaa katika manispaa ya mji wa Nga Pu Taw, kusini magharibi mwa jimbo la Ayeyarwady nchini Mynmar.
Vyombo vya habari nchini humo, vinasema kuwa vyakula na mimea mashambani imevamiwa na kulazimu mamlaka kuu nchini humo kuamua kuwalipa wananchi senti 4 kwa kila panya atakayeletwa kwa mamlaka akiwa ameuwawa.
Wanakijiji katika eneo la Ayeyarwady wamekuwa wakikabiliana na uvamizi huo wa panya kwa kuwaulia mbali wanyama hao ambao wamewavamia kwa wingi katika kipindi cha siku kumi zilizopita.
Maafisa wakuu wa eneo hilo wamelaumu mvua kubwa inayonyesha kwa sasa, jambo lililosababisha ongezeko kubwa la panya, huku wakivamia hifadhi ya chakula katika maghala ya wanakijiji.
Panya wengi wamepatikana kwenye nyumba 20, zilizoko karibu na vijiji vya Zee Chai village pwani ya manispaa ya Nga Pu Taw.
Kufikia sasa panya 800 wameuwawa, huku waliosalia wamekimbilia msitu ulioko karibu.
No comments:
Post a Comment