Zari na watoto wake.
Akizungumza na mtandao wa habari za udaku wa Kampala muda mfupi kabla ya kukwea pipa, Zari alisema kuwa, watu wanadhani atashindwa kuwalea watoto hao wa Ivan kwa kuwa ana wengine wawili aliozaa na mwanaume wake wa sasa, lakini si kweli kwani ana uhakika wa kuwalea watoto hao.
“Watu wanasema nitaweza? Wengine wanasema siwezi? Hapana, naweza. Siwezi kushindwa kuwalea wanangu, nitawalea mwenyewe,” alikaririwa Zari.
Baada ya kuondoka nchini Uganda, Zari alikwenda moja kwa moja na wanaye na kuweka makazi kwenye nyumba aliyonunua mpenzi wake wa sasa iliyopo jijini Johannesburg.
No comments:
Post a Comment