Kwa mujibu wa habari,mamlaka imesema kuwa watoto walikuwa wakichezea kombora hilo wakidhani kuwa ni mpira wa kuchezea wakati kombora hilo likÅŸlipuka.
Ripoti zinaonyesha kuwa bomu hilo aina ya Grenade liliokotwa na mtoto nje ya kambi na kuletwa ndani kwa ajili ya kuchezea.
Majeraha wote mpaka sasa wamefikishwa hospitalini.
Kambi ya IDP ipo katika kijiji cha Ari Adeye kaskazini mwa Lasanod.
Mpaka hivi sasa haijajulikana bado ni nani anahusika na kutupa bomu hilo ardhini.



No comments:
Post a Comment