44
Watu 44 wamejeruhiwa kutokana na moto uliolipuka katika magari ya kusafirishia mafuta mjini Alexandria nchini Misri.Katika taarifa iliyotolewa na msemaji wa wizara ya afya ya Misri, Khalid Mujahid imeeleza kuwa magari hayo yanayomilikiwa na shirika la petrolchemia yalilipuka wakati yalipokua yakisafirisha mafuta kutoka mjini Alexandria kuelekea Cairo na kujeruhi watu 44.
Mujahid aliongeza kuwa watu 6 kati majeruhi 44 wamejeruhiwa vibaya na kwamba takriban asilimia 60 ya sehemu za miili yao imeathiriwa kwa moto.



No comments:
Post a Comment