Na Anael James Waziri_Tall
Beki na nahodha msaidizi wa Manchester United Chris Smalling amsapoti Nahodha wa timu hiyo Wayne Rooney na kutamka huyo ndie mtu muhimu Zaidi..
Kauli hii imekuja baada ya Jumamosi Rooney kupigwa Benchi na Meneja
Jose Mourinho kwenye Mechi ya EPL, Ligi Kuu England, dhidi ya Mabingwa
wa England Leicester City ambayo Man United walishinda 4-1 huku Bao zao
zote zikifungwa Kipindi cha Kwanza.
Kuhusu kumtema Rooney, Mourinho alitoboa uchezaji wake umeathiriwa
na kupondwa mno wakati akiichezea England ambayo yeye pia ndie Kepteni
kama alivyo kwa Man United.
Mara baada ya Mechi hiyo na Leicester, Mourinho alipasua kuwa Wayne Rooney bado ni Mchezaji mkubwa kwa Timu yao.
Mourinho alisema ana imani yote kwa Rooney na kuwa bado ni Mchezaji muhimu kwa Timu yao licha ya kumuanzisha Benchi.
Hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Rooney kutoanza Mechi chini ya
Mourinho na mara ya mwisho kwa Kepteni huyo kupigwa Benchi ni Desemba 26
Mwaka Jana.
Mourinho alieleza: "Ni Mtu wangu, namuamini kwa kila kitu. Yeye ana furaha kama mimi na hii ndiyo Timu."
Aliongeza: "Yeye ni Mchezaji mkubwa kwangu mimi, United na ni Mchezaji mkubwa kwa Nchi hii!"
Kwenye Mechi hiyo na Leicester Rooney, ambaye wakati akiwa Benchi
alishangilia kila Goli la Man United kwa furaha kubwa, aliingizwa Dakika
ya 83 na kuzua mjadala mkubwa huko England na Dunia yote ya Soka
lakini, Smalling, ambae alivaa utepe wa Unahodha kwenye Mechi hiyo,
amesema hana wasiwasi Rooney atang'ara tena.
Smalling amesema: "Rooney alibaki yule yule kabla ya Gemu. Aliongea sana kama alivyo Siku zote."
"Bila kujali hali ilivyo, kwa Gemu yeyote ile bila kujali kapangwa
au la, Siku zote yeye ni Mtu yule yule tu. Ndio maana yeye ndie Mtu Mkuu
kwa England na Mtu Mkuu kwetu sisi!"
Smalling aliongeza: "Yeye ni Mtu mzoefu sana na amecheza michezo mingi Zaidi
na najua atarudia tena na kutingisha kwa sababu ana kipaji kikubwa!"
No comments:
Post a Comment