Na Mustafa Ismail
Chama cha Kidemocrasia nchini Gabon (PDG) kimekua kikitoa
zawadi za simu za mkononi, friji, mashine za kufua nguo na vifaa vinginevyo vya
matumizi ya nyumbani katika mji mkuu, Librevelle, kulingana na mwandishi wa BBC
idhaa ya kifaransa aliyeko mjini humo.
Zawadi hizo zilitolewa katika mkutano wa kisiasa
uliohudhuriwa na maelfu ya watu wanaharakati na wafuasi wa chama cha PDG.
Mwanamke mmoja, Naelle, ameiambia BBC:
" Sikuwa na lolote la kufanya, kwa hiyo nilienda.
Kulikuwa na msururu mrefu wa watu. Awamu yetu ilipofika, walitupatia zawadi,
lakini kwa masharti kwamba tujitambulishe .
Halafu wakatuwekea muhuri kwenye mikono yetu. Nilipokea simu
ya Ipad na jirani yangu akapewa friji."
Kwa hiyo kile ambacho watu wanafikiria kwa haya ni moyo wa
kutoa.
" Nadhani ilikua hivyo ili tumpigie kura Ali
Bongo", mwanamke mwingine kwenye mkutano huo , Gwenaelle, alimueleza
mwandishi wetu .
Kiongozi mkuu wa upinzani katika uchaguzi wa Jumamosi ni
Jean Ping, mkuu wa zamani wa Kamisheni ya Muungano wa Afrika.
Gabon ni mzalishaji mkuu wa mafuta , lakini theluthi tatu ya
raia wake wanaishi katika hali ya umaskini, kwa mujibu wa Benki ya Dunia.
No comments:
Post a Comment