NA ANAEL JAMES WAZIRI_TALL
Tetesi kutoka katika vyombo vya habari vya nchini Uingereza vinaripoti taarifa ya beki kisiki wa Mashetani wekundu Chriss Smalling kutimkia kwa Mzee Wenger.
Ikumbukwe kwamba Wenger aliwai kutaka kumsajili mchezaji huyu kabla hajaenda Manchester united. Mwaka 2010 Arsenal walikua na nafasi ya kumpata mchezaji huyu kutoka Fulham kabla ya pund milioni 10 za Manchester kukubalika.
Hadi sasa hii ni moja ya habari ambayo inakaa sana kwenye vichwa vya habari kuona kama kweli itawezekana kuona Smalling anahamia Arsenal. Jose Mourihno kocha ambae ni bingwa mchezo wa style ya kulinda lango lake, sio rahisi kumruhusu mchezaji huyu kuondoka lakini chochote kinaweza kutokea.
No comments:
Post a Comment