Tanzania wakiwa chini ya kocha wao mkuu Charles Boniface Mkwasa na nahodha wao Mbwana Samatta walikubali kupoteza kwa jumla ya goli 3-0, Zimbabwe ambao waliutawala mchezo kwa kiasi kikubwa walipata goli la kwanza dakika ya 9 kupitia kwa mshambuliaji wao anayecheza KV Oostende ya Ubelgiji Knowledge Musona.
Mchezo
ulienda mapumziko Zimbabwe wakiwa mbele kwa goli 1-0, lakini kipindi cha pili
Zimbabwe wakarudi na mpango mpya uliowasaidia kufunga magoli mawili dakika ya
54 kupitia kwa Mathew Rusike na Nyasha Mushekwi dakika ya 57.
Zimbabwe
wanaonekana kuwa imara zaidi ya Tanzania kwani wapo nafasi ya 110 katika
viwango vya FIFA na Tanzania wapo nafasi ya 144, kwa mechi 12 zilizopita
Tanzania alikuwa kapoteza mechi 5 huku akisha mechi 2 na kutoka suluhu mechi 5.
No comments:
Post a Comment