FIFA YAWEKA WAZI WAGOMBEA GOLI BORA LA MWAKA:SOMA HAPA UJUE NI YAPI YALIYOPENDEKEZWA - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Monday, November 21

FIFA YAWEKA WAZI WAGOMBEA GOLI BORA LA MWAKA:SOMA HAPA UJUE NI YAPI YALIYOPENDEKEZWA

HII Leo FIFA imetangaza Magoli 10 Bora kwa Mwaka 2016 ambayo yatapigiwa Kura ili kupata Goli Bora la Mwaka litakaloshinda Tuzo ya Puskas.
Image result for fifa
Wagombea hawa 10 sasa wanajumuika pia na Wagombea 23 wa Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani kwa Mwaka 2016 pamoja na Wagombea wengine wa Tuzo mbalimbali zikiwemo za Kocha Bora kwa Waume na Wake na Mchezaji Bora kwa Wanawake.
Magoli hayo 10 yanaweza kuangaliwa kwenye Mitandao ya FIFA FIFA.com/the-best na ule wa FIFA kwenye YouTube.
Magoli haya ni yale yaliyofungwa kuanzia Septemba 2015 hadi Septemba 2016.
Mashabiki wanaweza kupigia Kura Goli wanaloona ni Bora kati ya hayo 10 hadi Desemba 2 na baada ya hapo Magoli 3 Bora yataenda Fainali na Kura kwa Mashabiki zitaanza upya na kuendelea hadi Januari 9 na Mshindi kutangazwa huko Zurich hapo Januari 9, 2017 kwenye Hafla maalum ya kutoa Tuzo za FIFA za Ubora wa Mwaka.
Tuzo ya FIFA ya Puskas ilibuniwa Mwaka 2009 kumuenzi Ferenc Puskás, Nahodha na Staa wa Timu ya Taifa ya Hungary ya Miaka ya 1950.
MAGOLI 10 BORA YA MWAKA:
-Mario Gaspar (Spain) - 13.11.2015, Spain v. England, Kirafiki
-lompho Kekana (South Africa) - 26.03.2016, Cameroon v. South Africa, AFCON
-Marlone (Brazil) - 21.04.2016, Corinthians v. Cobresal, Copa Libertadores
-Lionel Messi (Argentina) - 21.06.2016, USA v. Argentina, Copa América
-Neymar (Brazil) - 08.11.2015, Barcelona v. Villarreal, La Liga (Spain)
-Saúl Ñíguez (Spain) - 27.04.2016, Atlético Madrid v. Bayern Munich, UCL
-Hal Robson-Kanu (Wales) - 01.07.2016, Wales v. Belgium, UEFA EURO 2016
-Daniuska Rodríguez (Venezuela) - 14.03.2016, Venezuela v. Colombia, South American U-17 Women’s Football Championship
-Simon Skrabb (Finland) - 31.10.2015, Gefle v. Ã…tvidaberg, Ligi Allsvenskan, Sweden
-Mohd Faiz Subri (Malaysia) - 16.02.2016, Penang v. Pahang, Malaysia Super League​
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
HABARI ZA AWALI:
FIFA MCHEZAJI BORA DUNIANI 2016: WAGOMBEA 23 WATAJWA, RONALDO, MESSI, IBRA, AGUERO, OZIL, ALEXIS..NDANI YA NYUMBA!
Friday, 04 November 2016 17:49
FIFALeo imetangaza Majina ya Wachezaji 23 Wagombea wa Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani kwa Mwaka 2016 na mbali ya wale wa kawaida, Cristiano Ronaldo na Lionel , pia wamoi Wachezaji 10 toka EPL, Ligi Kuu England, na Watatu kati yao wanatoka kwa Mabingwa wa England Leicester City.
Watatu hao ni Jamie Vardy, Riyad Mahrez na N'Golo Kante.
Wengine toka EPL ni Sergio Aguero, Kevin de Bruyne (Manchester City), Alexis Sanchez, Mesut Ozil (Arsenal), Paul Pogba, Zlatan Ibrahimovic (Manchester United) and Dimitri Payet (West Ham).
Listi hii ya Wagombea 23 itapungua na kubakizwa Wagombea Watatu watakaotangazwa Desemba 3.
Mshindi wa Tuzo hii atatajwa Januari 9 huko Zurich, Uswisi kwenye Hafla maalum.
Jana na Juzi FIFA ilitoa Majina ya Wagombea wa Tuzo za Ubora kwa Wanawake na pia Makocha Bora kwa Kinamama na Kinababa.

KURA KUPATA WASHINDI:
-Washindi wa Tuzo hizi watapatikana kwa Kura:
-Asilimia 50 ni ile ya Makepteni na Makocha wa Timu za Taifa za Nchi Wanachama FIFA
-Asilimia 25 ya Kura itatoka kwa Kura za Mtandaoni za Mashabiki
-Asilimia 25 ni Kura za Wawakilishi 200 wa Wanahabari kutoka Mabara yote 6 Duniani.

WAGOMBEA 30 - Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani 2016:
Sergio Aguero (Manchester City), Gareth Bale (Real Madrid), Gianluigi Buffon (Juventus), Cristiano Ronaldo (Real Madrid), Kevin De Bruyne (Manchester City), Antoine Griezmann (Atletico Madrid), Zlatan Ibrahimovic (Manchester United), Andres Iniesta (Barcelona), N'Golo Kante (Chelsea), Toni Kroos (Real Madrid), Robert Lewandowski (Bayern Munich), Riyad Mahrez (Leicester City), Lionel Messi (Barcelona), Luka Modric (Real Madrid), Manuel Neuer (Bayern Munich), Neymar (Barcelona), Mesut Ozil (Arsenal), Dimitri Payet (West Ham), Paul Pogba (Manchester United), Sergio Ramos (Real Madrid), Alexis Sanchez (Arsenal), Luis Suarez (Barcelona), Jamie Vardy (Leicester City).
WACHEZAJI –  WANAWAKE, Wagombea 10:
Camille Abily: Kiungo; 31; France and Lyon
Melanie Behringer: Kiungo; 30; Germany and Bayern Munich
Sara Dabritz; Kiungo, 21; Germany and Bayern Munich
Amandine Henry; Kiungo; 27; France and Portland Thorns
Saki Kumagai: Beki; 26; Japan and Lyon
Carli Lloyd; Kiungo; 34; USA and Houston Dash
Dzsenifer Marozsan; Kiungo; 24; Germany and Lyon
Marta; Fowadi; 34; Brazil and FC Rosengard
Lotta Schelin; Fowadi, 32, Sweden and FC Rosengard
Christine Sinclair; Fowadi; 33; Canada and Portland Thorns
MAKOCHA –  WANAUME, Wagombea 10:
* Chris Coleman (Wales/Welsh national team)
* Didier Deschamps (France/French national team)
* Pep Guardiola (Spain/FC Bayern Munich/Manchester City)
* Jürgen Klopp (Germany/Liverpool)
* Luis Enrique (Spain/FC Barcelona)
* Mauricio Pochettino (Argentina/Tottenham Hotspur)
* Claudio Ranieri (Italy/Leicester City)
* Fernando Santos (Portugal/Portuguese national team)
* Diego Simeone (Argentina/Atlético Madrid)
* Zinédine Zidane (France/Real Madrid).
MAKOCHA –  WANAWAKE, Wagombea 10:
* Philippe Bergeroo (France/French national team)
* Jill Ellis (USA/US national team)
* John Herdman (England/Canadian national team)
* Silvia Neid (Germany/German national team)
* Vera Pauw (Netherlands/South African national team)
* Gérard Prêcheur (France/Olympique Lyonnais)
* Pia Sundhage (Sweden/Swedish national team)
* Oswaldo Vadão (Brazil/Brazilian national team)
* Martina Voss-Tecklenburg (Germany/Swiss national team)
* Thomas Wörle (Germany/FC Bayern Munich).
FIFA – Tuzo za Ubora zitakazotolewa:
-Mchezaji Bora Duniani 2016 [The Best Fifa Men's Player 2016]
-Mchezaji Bora Duniani 2016 kwa Kinamama [The Best Fifa Women's Player 2016]
-Kocha Bora kwa Wanaume 2016 [The Best Fifa Men's Coach 2016]
-Kocha Bora kwa Wanawake 2016 [The Best Fifa Women's Coach 2016]
-Tuzo ya Puskas 2016 kwa Goli Bora [The Fifa Puskas Award 2016 for goal of the year]
-Tuzo ya Uchezaji wa Haki 2016 [The Fifa Fair Play Award 2016]
-Tuzo ya Mashabiki 2016 [The Fifa Fan Award]

Source:Soka in Bongo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here