ANGALIA WALICHOSEMA MOURINHO NA ROONEY PAMOJA NA GUARDIOLA NA YAYA TOURE BAADA YA MECHI - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Sunday, November 20

ANGALIA WALICHOSEMA MOURINHO NA ROONEY PAMOJA NA GUARDIOLA NA YAYA TOURE BAADA YA MECHI

MARA baada ya Mechi za Jana za EPL, Ligi Kuu England, baadhi ya Wadau wa Mechi hizo walitoa matamshi mbalimbali yenye mvuto kwa Washabiki.
Image result for mourinho vs guardiola

Baadhi ya hao ni Mameneja wa Man City Pep Guardiola na Mchezaji wake Yaya Toure aliempiga marufuku kucheza na ghafla Jana kumchezesha na Staa huyo kupiga Bao zote 2 na kuwapa ushindi City wa 2-1 dhidi ya Crystal Palace.
 
Pia Jose Mourinho, Meneja wa Man United ambae Jana walipokwa ushindi baada Arsenal kusawazisha Dakika ya 89 na kupata Sare 1-1 lakini hilo limeendeleza Rekodi ya Mourinho kutofungwa na Arsene Wenger katika Mechi 15 za EPL ambazo ameshinda 8 na Sare 7.
 
Vile vile, Nahodha wa Man United Wayne Rooney ambae pia ni Nahodha wa Timu ya Taifa ya England aliongea kuhusu kusakamwa sana kwake.
NINI WAMESEMA?
-WAYNE ROONEY: 
Wayne Rooney amedai amekuwa akisakamwa mno wakati akiichezea England na hilo ni tendo la fedheha kubwa.
Rooney ameichezea England Mechi 119 akiwa ni wa pili katika Historia kwa kucheza Mechi nyingi nyuma ya Kipa Peter Shilton aliecheza Mechi 125 na pia ndie Mfungaji Bora katika Historia ya Nchi hiyo.
Hivi karibuni Jarida moja huko England lilitoa Picha za Rooney akinywa Pombe Hotelini waliyokuwa wakikaa Timu ya England ingawa Siku hiyo Kikosi chote kilikuwa kimepewa Ofu na Meneja Gareth Southgate.
 
Akiongea hapo Jana mara baada ya Mechi ya Man United na Arsenal, Rooney aliwashambulia wanaomsakama na kudai wanakosa heshima.
 
Alisema: "Inaonyesha kama Wanahabari wanaandika Wasifu wa Kifo changu na hilo sitaruhusu litokee. Yanayotokea ni fedheha. Napenda kuchezea Nchi yangu na naskia fahari mafanikio yangu. Bado sijaisha!"
Nao Wachezaji wa zamani wa England, Ian Wright na Alan Shearer, wamejitokeza kumpa sapoti Rooney.
Akiongea hapo Jana, Ian Wright, alisema: "Kwa Miaka Mitatu au Minne wamekuwa wakimshambulia. Nimefurahi mno sasa anajibu mapigo. Pigana Wayne!"
 
Nae Nahodha wa zamani wa England Alan Sherer amesema: "Siku zote amejitolea kwa nguvu zote kuichezea England. Kama alipewa Ofu na kuamua kubaki Hotelini na kupata kinywaji hakufanya kosa labda ingekuwa ameenda kinyume na Meneja!"
 
-YAYA TOURE:
Mara baada ya Jana kuchezeshwa kwa mara ya kwanza baada Miezi Mitatu baada kupigwa stopu na Meneja Pep Guardiola kufuatia ugomvi na Wakala wake, Yaya Toure ambae alifunga Bao zote 2 wakati Man City inaifunga Crystal Palace 2-1 amefunguka na kusema hakushangazwa kuitwa kuichezea tena Timu hiyo.
Toure, mwenye Miaka 33, ameeleza: "Nilikuwa tayari kiakili na nilijua ipo Siku Meneja ataniita!"
Toure, ambae ameiwezesha City kutwaa Ubingwa EPL mara 2, Jana alipokewa vizuri na Mashabiki wa Timu hiyo waliokuwa wakimuimba Mechi nzima.
Mwishoni mwa Mechi hiyo na Palace Wachezaji wote wa City walimshangilia Toure na kumsindikiza kwa Makofi hadi nje ya Uwanja.
 
-JOSE MOURINHO:
Kwa mujibu wa Meneja wa Man United Jose Mourinho Timu yao ndio Timu ambayo haina bahati baada ya Jana Arsenal kusawazisha Dakika ya 89 na kupata Sare ya 1-1.
 
Mourinho ameeleza: "Sina la kusema kuhusu Wachezaji wangu lakini nawaonea ruhuma kwani hiyo ni kama tumefungwa wakati Arsenal wanaona wameshinda!"
Aliongeza: "Sare hizi na Burnley, Stoke na Arsenal ni kupoteza Pointi 9. Tungepata Pointi 6 tu tuko 4 Bora na karibu ya kileleni! Tunajua hivi sasa sie ndio Timu isiyo na bahati kwenye EPL!"
Man United wameshapambana na Manchester City, Liverpool, Chelsea na Arsenal bila ushindi wakitoka Sare 3 na kufungwa na Chelsea tu.
 
Hivi sasa wapo Nafasi ya 6 wakiwa Pointi 5 nyuma ya Arsenal ambao wako Nafasi ya 4 na ambao wapo Pointi 2 nyuma ya Vinara Liverpool.

source:soka in bongo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here