JUMANNE Usiku England watacheza
Mechi ya Kimataifa ya Kirafiki Uwanjani kwao Wembley Jijini London dhidi ya
Spain na Kepteni wao Wayne Rooney hataanza Mechi hii.
Kwa mujibu wa Kocha wa Muda wa
England, Gareth Southgate, hatamuanzisha Rooney na Utepe wa Unahodha utavaliwa
na Nahodha wa Liverpool Jordan Henderson.
Henderson, Mwenye Miaka 26, alikuwa
ndie Nahodha wa England walipotoka Sare 0-0 Ugenini na Slovenia Mwezi
uliopita wakati Rooney alipoanzia Benchi.
Hii Leo, Rooney, ambae Ijumaa
aliiongoza Timu yao kuitandika 3-0 Scotland katika Mechi ya Kundi ya kusaka
kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 huko Russia, hakufanya Mazoezi
na Kikosi cha England ikisemekana ana maumivu kidogo.
Hapo Kesho Jumanne zipo Mechi nyingi
za Kimataifa za Kirafiki na zamvuto ni pamoja na Italy kucheza na Mabingwa wa
Dunia Germany na France kuwavaa Mabingwa wa Afrika Ivory Coast huko Stade
Bollaert-Delelis, Mjini Lens Nchini France.
Mechi za kesho Jumanne
Mechi za kesho Jumanne
Novemba 15
14:00 Jordan v Lebanon
14:00 Bahrain v Kyrgyzstan
16:00 Kenya v Liberia
17:00 Morocco v Togo
17:00 Tunisia v Mauritania
17:00 Gabon v Comoros
18:00 Tunisia v Mauritania
19:00 Russia v Romania
21:00 Malta v Iceland
21:45 Hungary v Sweden
22:00 Ukraine v Serbia
22:30 Czech Republic v Denmark
22:45 Northern Ireland v Croatia
22:45 Italy v Germany
22:45 Austria v Slovakia
23:00 France v Ivory Coast
23:00 England v Spain
No comments:
Post a Comment