MENEJA wa Manchester City, Pep
Guardiola amesema itakuwa vigumu kwa kikosi chake kuwafukuzia vinara wa Ligi
Kuu Chelsea katika mbio za ubingwa.
City wamekwea mpaka nafasi ya pili
katika msimamo wa ligi baada ya kuichapa Hull City kwa mabao 3-0 jana na kuwafanya
kuwa nyuma ya Chelsea kwa tofauti ya alama saba.
Akihojiwa Guardiola amesema
wamecheza mechi saba zaidi ya Chelsea hiyo ndio sababu haswa ni kwanini anaona
itakuwa vigumu kuwakuta.
Meneja huyo aliendelea kudai kuwa Liverpool
ilikaribia kutwaa taji kipindi cha hivi karibuni kwasababu walikuwa wana
mchezaji mmoja pekee kwa wiki na msimu uliopita ilikuwa hivyohivyo kwa
Leicester City.
Guardiola amesema kuwa msimu huu
Chelsea na Liverpool ndio nafasi yao kwasababu hawana majukumu mengi.
No comments:
Post a Comment