Yanga
imefanikiwa kupitisha jina la mshambuliaji wa zamani wa Zesco, Winston Kalengo.
Kalengo
ametua Yanga baada ya jina lake kuwasilishwa katika nusu saa ya mwisho kabla ya
dirisha ya usajili.
Taarifa
zinaeleza, Yanga imepitisha jina hilo la Kalengo anayechukua nafasi ya Mzambia,
Obey Chirwa.
Yanga
imemrudisha Chirwa FC Platnums kwa mkopo, safari hii akiwa analipwa nusu
mshahara na Yanga na Wazimbabwe hao watamlipa nusu mshahara.
Mjadala
mkubwa kuhusiana na hilo, ndiyo ulichelewesha Yanga kuwasilisha jina hilo
katika hatua za mwisho na imeelezwa Yanga wameliwasilisha katika majina ya
wachezaji wao saa 5:36, ikiwa ni dakika 24 kabla ya usajili huo wa dirisha dogo
kufungwa.
Pamoja
na kufanya vizuri Zambia akiwa na Zesco, Kalengo aliwahi kucheza soka la
kulipwa nchini Congo Brazaville na anaelezwa kuwa mkali wa kupiga mashuti,
mwenye njaa ya mabao.
No comments:
Post a Comment