Katika
mechi hiyo iliyomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Amaan mjini
Zanzibar, Azam FC walicheza vizuri lakini walipoteza nafasi nyingi.
Lakini
Franka Domayo ‘Chumvi’ ndiye alifunga bao safi kwa shuti kali nje ya 18
akifunga bao hilo katika dakika ya 33. Domayo, kiungo wa zamani wa
Yanga, ndiye ameibuka kuwa nyota wa mchezo huo.
Azam FC ingeweza kupata mabao zaidi, lakini washambuliaji wake hawakuwa makini katika umaliziaji.
No comments:
Post a Comment