SHIRIKISHO LA SOKA DUNIANI FIFA WAMEONGEZA TIMU SHIRIKI KOMBE LA DUNIA,HABARI ZOTE HAPA - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Tuesday, January 10

SHIRIKISHO LA SOKA DUNIANI FIFA WAMEONGEZA TIMU SHIRIKI KOMBE LA DUNIA,HABARI ZOTE HAPA

 
SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limeamua kuongeza michuano ya Kombe la Dunia kutoka timu 32 mpaka kufikia timu 48.

Katika mpango huo kutakuwa na makundi 16 yenye timu tatu ambapo timu mbili ndio zitasonga mbele katika hatua ya mtoano ya 32 bora.

Idadi ya mechi inatarajiwa kuongezeka mpaka kufikia mechi 80 kutoka 64 lakini washindi bado watacheza mechi saba kama ilivyokuwa awali.

Michuano hiyo itakuwa ikifanyika ndani ya siku 32 na itakuwa ni mara ya kwanza kufanyika kwa mabadiliko kama hayo toka mwaka 1998.

Kombe la Dunia Timu
1930 Uruguay 13
1934 Italy 16
1950 Brazil 13
1954 Switzerland 16
1958 Sweden 16
1974 West Germany 16
1982 Spain 24
1986 Mexico 24
1998 France 32

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here