LABU ya
Manchester United inadaiwa kuwa tayari kuongeza mkataba wa mwaka mmoja uliopo
katika mkataba wa David de Gea ili kuwakatisha tama Real Madrid.
De Gea
ambaye alisaini mkataba wa mpaka 2019 baada ya kushindwa kwenda Santiago
Bernabeu Septemba mwkaa 2015, sasa ataongezwa mkataba wa mwaka mmoja zaidi
pamoja na nyongeza ya mshahara.
Kwasasa De
Gea analipwa paundi 180,000 kwa wiki na kama akiongezwa mkataba huo utashuhudia
akikunja kitita cha paundi 200,000 kwa wiki.
Taarifa
kutoka nchini Uingereza zimedai kuwa hakutakuwa na tatizo lolote katika
nyongeza ya mkataba huo.
No comments:
Post a Comment