Jamii Mkoani Shinyanga imekumbushwa kuwa ina wajibu
mkubwa wa kuhakikisha inaweka mazingira
salama kwa watu wenye albinism ili kuliwezesha kundi hilo kuwa huru lenye
amani,katika nchi yao.
Mwakilishi wa Jeshi la Polisi kamishina Msaidizi Mussa,ametoa wito huo wakati wa uzinduzi wa mradi wa
kuelimisha Jamii utakaotekelezwa na chama cha watu wenye ualbinism,ambapo
amesema Jamii itambue umuhimu wa kuthamini Kundi hilo ili liweze kuwa
huru,salama na lenye amani,kuliko hivi sasa ambapo wanauawa kutokana na imani
Potofu.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa chama cha watu wenye albinism Mkoa wa Shinyanga
Mwalimu Martin Luben ameiomba Jamii
kuthamini na kuheshimu utu wa albino kwani ni binaadamu wenye haki na mahitaji
sawa na wengine,badala ya kuwa na hofu.
Mradi wa kuelimisha Jamii kuondokana na imani Potofu za kishirikina zinazosababisha
Mauaji ya watu wenye ualbino umezinduliwa leo kwenye Hotel ya Empire mjini Shinyanga na kuhusisha shirikisho la vyama
vya watu wenye ulemavu SHIVYAWATA,Wadau,wanasheria
Jeshi la Polisi,waganga wa Jadi na vyombo vya habari.
Mradi huo utatekelezwa na chama cha watu wenye ualbino Mkoa
wa Shinyanga,chini ya ufadhiri wa Shirika la OPEN SOCIETY INITIATIVE FOR EAST AFRIKA,ambao utatekelezwa kwa kipindi cha mwaka mmoja katika mkoa
wa Shinyanga.
No comments:
Post a Comment