TIMU ZA ONGEZEKA KUSHIRIKI KOMBE LA DUNIA 2018,HABARI KAMILI HAPA - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Thursday, December 8

TIMU ZA ONGEZEKA KUSHIRIKI KOMBE LA DUNIA 2018,HABARI KAMILI HAPA

Image result for infantino
RAIS wa FIFA Gianni Infantino ana matumaini kuwa Fainali za Kombe la Dunia huko mbeleni zitakuwa na Makundi 16 ya Timu Tatu Tatu kwenye Mashindano yakatakayokuwa na Jumla ya Timu 48.

Awali Infantino, ambae alitwaa wadhifa wa Rais wa FIFA Mwezi Februari, alizungumzia kuwepo Timu 32 hadi 40.
Kwenye Plani hii ya sasa ya Makundi 16, Timu 2 za juu za kila Kundi ndizo zitasonga na kuunda Makundi mengine ya Timu 32 na kisha baada ya hapo Mashindano kuendelea kwa kufuuatia Raundi za Mtoano hadi Fainali.

Uamuzi huu wa kutumia Mfumo mpya utafanywa Mwezi Januari lakini kutumika kwake kutaanzia Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2026.

Ikiwa Mfumo huo wa Makundi 16 ya Timu Tatu Tatu hautapita yapo mapendekezo kadhaa ya Mifumo tofauti ambayo ni:
-Fainali za Timu 48 lakini awali Timu 32 zitacheza Mtoano wa Mechi 1 tu ili kupata Timu 16 ambazo zitaungana na Timu 16 nyingine ambazo zinapita moja kwa moja bila kucheza Mtoano ili kufanya Jumla ya Timu 32 kama ilivyo Fainali za Kombe la Dunia za sasa.

-Mfumo mwingine ni wa kuwa na Fainali ya Timu 40 ambazo zitakuwa na Makundi 10 ya Timu 4 kila moja au Makundi 8 ya Timu 5 kila moja.

Mara ya mwisho kwa idadi ya Timu zinazocheza Fainali ya Kombe la Dunia kuongezwa ilikuwa ni Fainali za 1998 zilipoongezwa kutoka Timu 24 hadi 32.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here