KIUNGO wa
zamani wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Chelsea, Frank Lampard anatarajiwa
kupewa nafasi katika benchi la ufundi la timu ya taifa ya Uingereza.
Taarifa hizo
za kocha mpya wa Uingereza Gareth Southgate kumtaka Lampard zimekuja saa chache
baada ya taarifa rasmi kuwa Sammy Lee ameachia rasmi wadhifa wake wa kocha
msaidizi.
Southgate
anataka kuunda jopo lake mwenyewe na anaona Lampard kama mtu atakayemfaa katika
benchi lake.
Lampard
ambaye alistaafu soka la kimataifa muda mfupi baada ya michuano ya Kombe la
Dunia mwaka 2014, ndio kwanza ameondoka New York City FC kufuatia kumaliza
mkataba wake.
No comments:
Post a Comment