Arsene Wenger amesema Arsenal haitawauza Alexis Sanchez na
Mesut Ozil hata kama hawatasaini Mikataba Mipya.
Masta hao wakubwa ambao ni tegemezi kubwa kwa
Arsenal wamebakiza Miezi 18 katika Mikataba yao ya sasa lakini mpaka sasa
hawajaafiki kusaini Mikataba Mipya ya Nyongeza.
Sanchez na Ozil wanataka Nyongeza kubwa ya
Mishahara yao ili wavune kama Mastaa wengine wakubwa lakini Menejimenti ya
Arsenal imekataa hilo.
Wawili hao, Msimu huu wameifungia Arsenal Jumla
ya Mabao 21.
Akiongelea hali ya sasa, Wenger ameeleza: “Hata
iweje watabaki kwa Miezi 18 iliyobaki na labda zaidi ya hapo.”
Aliongeza: “Wachezaji hawa watabaki si chini ya
Miezi 18 lakinimmazungumzo yanaendelea lakini si ya kuwekwa wazi.’
Ingawa Wenger ana matumaini makubakia kwa Ozil na
Sanchez lakini ameshindwa kuwapa uhakika wowote Mashabiki wa Arsenal.
Alipohojiwa kama anawapa uhakika Mashabiki kuhusu
kubakia kwa Wawili hao, Wenger alijibu: “Hapana. Wana Miezi 18 ya Mikataba yao
na wataendelea kucheza wakiwa hapa. Baada ya hapo itabidi Mikataba iongezwe
lakini siwezi kuzungumzia suala katika kila Mahojiano na Wanahabari. Ni kawaida
mkiongeza Mkataba kuna majadiliano.”
Hivi Sanchez anahusishwa na kuhamia huko
Mashariki ya Mbali, hasa China, ambako imeripotiwa amepewa Ofay a ajabu ya
kulipwa Pauni Laki 4 kwa Wiki.
Wenger amepasua: “Naamini hilo.
No comments:
Post a Comment