WAISLAMU WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUADHIMISHA MAZAZI YA MTUME - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Wednesday, December 7

WAISLAMU WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUADHIMISHA MAZAZI YA MTUME

Na Mustafa Ismail
Waislamu wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho ya sherehe za maulid  ya kuadhimisha mazazi ya bwana mtume Muhammad [s.a.w] ili kuonesha umoja na mapenzi kwa mtume 

Akiongea na waandishi wa habari jijini dar es salaam sheikh mkuu wa mkoa huo Alhadi Musa Salum amewatakawaislamu kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo yatakayofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja siku ya juma pili ya tarehe 11/3/1438 hijriya sawa na 11/12/2016 miladiya

“Ndugu waandishi wa habari tumewaita kwa jambo moja kubwa waislamu duniani kote hivi sasa wanatarajia kupokea mazazi au kuzaliwa kwa kiongozi wao mtume Muhammad [S.A.W]lakini pia kubwa tunalotaka kulizungumzia ni sherehe hizo kimkoa zitafanyika katika viwanja vya mnazi mmoja siku ya jumapili ya tarehe 11/12/2016 kuanzia saa mbili usiku.”

Sheikh Alhadi alisema kuwa mauled itasindikizwa na maandamano  yatakayoa anza katika viwanza vya mnazi mmoja na kupita katika barabara kadhaa jijini humo “ lakini pia shughli hiyo itaandamana na maandamano yatakayoanza alasiri katika viwanja vya mnazi mmoja kupitia morogoro road yatapitia katika barabara ya msimbazi yatatokea barabara ya uhuru na kutokea katika barabara ya Lumumba na kurudi tena katika viwanja vya mnazi mmoja.”

Aidha Sheikh Alhadi aliwaomba waislamu wa mkoa wa Dar es salaam kusherehekea sikukuu hiyo kwa amanai na utulivu na kwa namna itakayomridhisha mola  wao huku akiwataka kujiepusha na uvunjaji wa sheria na kuwataka kulinda umoja amani na mshikamano.

Mgeni rasmi katika shere hiyo atakuwa Rais mstaafu wa awamu ya pili Alhajj Ali Hassan Mwinyi ambaye ataongozana na viongozi wa vyama mbalimbali naviongozi wa kidini.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni muislamu jitambue badilika aamani ndio maisha yetu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here