Sote tunajua taabu inayopatikana ya ubebaji Begi au mabegi pale tunaposafiri kuelekea katika kituo aidha cha Mabasi, Treni au Ndege.
Adha hiyo sasa inakaribia kuondoka kabisa baada ya kufanyika mageuzi makubwa ya kiteknolojia kwa kuundwa begi la kisasa.
Travelmate ndio begi la kwanza duniani ambalo linatembea lenyewe bila kubebwa kuelekea kule ambapo muhusika wa begi anapoelekea.
Begi hilo la aina yake linalofanya safari iwe rahisi lilizinduliwa na Travemate mwaka 2016 mwezi oktoba.
Ni begi linalotumia Teknolojia ambayo hutakuwa na kazi ya kulibeba bali litakuwa linakufuata popote uendapo.
Ili liweze kufanya kazi vizuri na kumfuata mwenye begi limeunganishwa na simu kupitia GPS ili kuweza kumfatilia mmiliki wake kwa usahihi zaidi. Popote utakapoliweka utaweza kulifuatilia
kupitia GPS.
No comments:
Post a Comment