Suala la kujitenga kwa ukanda huo wa Pwani limezua mjadala mkubwa sio tu katika ukanda huo bali taifa la Kenya kwa Ujumla ambapo inaelezwa kuwa hii si mara ya kwanza, gumzo kama hilo kuyumbisha siasa za taifa hilo.
Kenya huenda ikakwama kwa muda mrefu katika sintofahamu ya kisiasa, kikatiba na kiuchumi kufuatia mgogoro uliojitokeza baada ya uchaguzi wa marudio ambapo jana Kiongozi wa upinzani nchni humo Raila Odinga ambaye hvi sasa yuko ziarani nchni Marekani alipendekeza serikali ya muda iundwe na kutawala kwa muda wa miezi sita kama sehemu ya kutatua mzozo huo.



No comments:
Post a Comment