Kesi dhidi hamisa na msanii diamond kutolewa uamuzi kesho. - MKWELITZ BLOG

Breaking

.

.

.

.

Thursday, November 9

Kesi dhidi hamisa na msanii diamond kutolewa uamuzi kesho.


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kesho Novemba 10, 2017 inatarajia kutoa uamuzi dhidi ya kesi ya matunzo ya mtoto iliyofunguliwa na mwanamitindo Hamisa Mobeto dhidi ya msanii maarufu nchini, Nassib Abdul au Diamond Platinum.

Uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi, Devotha Kisoka upande wa Watoto.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mahakama kusikiliza hoja za pande zote husika kutokana na.msanii Diamond kuwasilisha pingamizi kupinga kesi hiyo kwa madai kuwa kesi hiyo imefunguliwa kwa kutumia kifungu ambacho si sahihi.

Mwezi uliopita, Mwanamitindo Hamisa alifungua kesi hiyo mahakamani hapo akiiomba mambo mbalimbali likiwemo la matunzo ya mtoto waliozaa na msanii huyo.

Katika kesi hiyo, Hamisa alifungua kesi hiyo kupitia mawakili wake Abdullah Lyana na Walter Godluck kutoka kampuni ya uwakili ya Century Attorneys ambapo anaiomba mahakama imwamuru Diamond kutoa matunzo ya mtoto ya kila mwezi.Kupitia hati hiyo ya madai, mwanamitindo huyo anaomba Diamond amuombe msamaha kwa kumsababishia madhara yaliyoishtua familia yake.

Hata hivyo, Diamond aliwasilisha hati ya majibu kinzani akipinga maombi hayo ya Diamond akidai gharama anazodai kulipwa kwa mwezi sh. milioni tano kwa ajili ya matunzo ya mtoto ni kubwa hawezi kuzimudu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here