Na Annel James
KIUNGO
Mjeruman wa Manchester United, Bastian Schweinsteiger amejumuishwa katika
kikosi cha wachezaji 25 wa klabu hiyo kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu.
Katika
siku za karibuni kulikuwa na taarifa kuwa meneja wa United Jose Mourinho
alikuwa amemuhabalisha kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32 kuwa anaweza
asiichezee tena.
Nahodha
huyo wa zamani wa Ujerumani amestaafu soka lake la kimataifa mapema wiki hii
baada ya kufunga mabao 24 katika mechi 121 alizoichezea. Klabu zote 20 za
Ligi Kuu zilipaswa kuwasilisha majina ya wachezaji 25 watakaowatumia katika
Ligi Kuu, jana.
Schweinsteiger ambaye alisaini mkataba wa miaka mitatu
Julai mwaka jana, amekuwa akifanya mazoezi peke yake na kikosi cha vijana chini
ya umri wa miaka 23 toka Mourinho akabidhiwe mikoba kiangazi hiki.
No comments:
Post a Comment