Kampuni ya
mtandao ya Tigo leo imekabidhi madawati
185 yenye thamani ya shilingi milioni 31 yatakayogawiwa kwa shule nne katika mkoa wa Geita ikiwa
ni sehemu ya mkakati wake unaoendelea nchi nzima wa kutoa msaada wa
madawati ambayo yatainufaisha mikoa mine kwenye tamasha la fiesta 2016
Akizungumza
katika sherehe za kukabidhi madawati hayo zilizofanyika katika Shule ya
Msingi Mwatulole, Meneja wa Kikanda wa Tigo Kanda ya Ziwa Edgar Mapande,
alisema kuwa umekuwepo uhitaji mkubwa wa madawati katika shule za msingi
na kutokana na kuwepo kwa uhaba wa madawati imebainika kuwa ni moja
ya sababu zinazoathiri uwezo wa kujifunza pamoja na ufanisi wa masomo
miongoni mwa wanafunzi katika shule zetu nyingi za msingi.
“Lengo letu
kama kampuni ni kuhakikisha kuwa tunaboresha mazingira ya kujifunzia katika
shule zetu za msingi na tunayo furaha kwamba msimu wa FIESTA 2016 unaleta
mabadiliko kwa kizazi cha baadaye ambacho ni wanafunzi walio katika
shule za msingi kwa kuhakikisha hawakai tena chini sakafuni,” alisema Mapande.
Makabidhiano
ya madawati hayo yalishuhudiwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu
Ezekiel Kyingu ambaye alisema kuwa madawati hayo
185 yataboresha kwa kiwango kikubwa mazingira ya kujifunza kwa
watoto katika mkoa huo na kutoa witom kwa watu wengine wenye mapenzi
mema kujitokeza na kujiunga na juhudi hizo za kuondoa uhaba wa madawati
uliobakia katika mashule mkoani humo.
Kyingu
alizitaja shule zitakazonufaika na madawati hayo na idadi
yake katika mabano kuwa ni Mwatulole (50), Nyankumbu (45), Ukombozi (45),
na Kivukoni (45).
“Tunawashukuru
sana Tigo kwa kutuunga mkono katika juhudi zetu kwa kupunguza idadi ya
uhaba wa madawati katika shule za msingi mkoani Geita. Tunaamini
madawati haya 185 yatatufikisha mbali katika kuwawezesha
mamia ya watoto kuwa katika mazingira mazuri ya kujifunzia yanayotakiwa kwa
ajili ya mafanikio katika kuelekea kuwa viongozi wa baadaye,” alisema Kyingu.
Hadi sasa
tigo ishatoa msaada wa madawati kwa mkoa wa kagera na Kahama
jukumu la kusukuma gurumu la elimu nijukumu la kila mtanzania hivyo basi tushirikiane katika kuhakikisha vijana wetu wanapata elimu bora na sio bora elimu kwa kuchangia madawati kwa namna moja au nyengine
No comments:
Post a Comment