Na Anael James Waziri_Tall
Clattenburg
ametangazwa kuwa mwamuzi wa mchezo wa mwishoni wa wiki hii ambao utawakutanisha
mahasimu wa jiji la Manchester.
Mchezo huo
utazikutanisha Manchester City inayoongozwa na Pep Guardiola na Manchester
United ya Jose Mourinho huku timu zote zikiingia katika mchezo huo zikiwa
hazipoteza mchezo toka kuanza kwa msimu huu.
Mike Dean
ameteuliwa kuwa mwamuzi wa ziada huku Jake Collins na Steve Bennett
wakitarajiwa kushika vibendera kumsaidia Clattenburg.
Clattenburg
ndio mwamuzi aliyechezesha fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu
wa 2015-2016 na ile ya Ulaya iliyochezwa mapema kiangazi hiki.
No comments:
Post a Comment