Ikiwa zimebaki siku mbili tu kupigwa kwa darby ya Manchester maneno yamezidi kuwa mazuri kiasi kwamba kutia morali kwa mashabiki wa soka Duniani.
Streka wa Manchester UNITED Ibrahmovic amempa onyo Goli kipa mpya wa Machester CITY Claudio Bravo kuwa ajiandae kupokea kipigo kutoka kwake,na kumtumia vifaa vya michezo ikiwemo kiatu alichokuwa akitumia katika mazoezi kupitia mtandao wa kijamii wa Facebook na Kumtag kiasi kwamba awe makini katika mchezo huo.
Ibrahmovic akiwa ndiye kinara wa magoli katika klabu yake ya Manchester UNITED akiwa ameifungia magoli matatu katika mechi zake tatu kwenye ligi kuu Uingeleza atakutana na Mahasimu wao katika Dimba la OLD TRAFFORD jumamosi mchana.
Manchester United inatarajia kumkosa Beki wao wa kushoto LUKE SHAW aliyeumia kwenye mechi ya kimataifa kati ya timu yake ya Taifa ya England ilipocheza na Slovekia, na Sambamba na beki wa kulia ANTONIO VALENCIA ambaye Timu yake ya Taifa itakapocheza mchezo leo usiku na kama atapewa muda wa kupumzika na kocha Jose Mournho kutakuwa na uwezekano wa kumkosa katika mechi hiyo na itambidi kumtumia Daley Blind kama beki wa kushoto na Darmian kama Beki wa Kulia.
RATIBA LIGI KUU ENGLAND
Saa za Afrika Mashariki
JUMAMOSI SEPTEMBA 10
14:30 Man United v Man City
17:00 Arsenal v Southampton
17:00 Bournemouth v West Brom
17:00 Burnley v Hull
17:00 Middlesbrough v Crystal Palace
17:00 Stoke v Tottenham
17:00 West Ham v Watford
19:30 Liverpool v Leicester
JUMAPILI SEPTEMBA 11
18:00 Swansea v Chelsea
22:00 Sunderland v Everton
No comments:
Post a Comment