Na Anael
James
Kocha Mkuu
wa Yanga, Hans van der Pluijm amesema wanachotakiwa ni ushindi kwa mechi zaidi
ya mbili zijazo ili kujiweka sawa kwamba sasa wamerejea kwenye ligi.
Pluijm raia
wa Uholanzi amesema ushindi wa mechi moja, hauwatoshi ni lazima washinde ili
kuinua morali na kuweka hisia mpya ndani ya kikosi hicho.
“Lazima
turudishe morali miongoni mwetu, tunatakiwa kuhakikisha tunashinda mfululizo
halafu tutajiweka sawa,” alisema.
“Tunajua
ligi itakuwa ngumu, lakini nguvu ya ushindi itaongezeka kila tunaposhinda na
kuinua morali.”
Yanga
inaingia kambini kesho tayari kwa maandalizi ya mwisho dhidi ya Ndanda FC
katika mechi yake ya pili ya ligi kuu Tanzania.
No comments:
Post a Comment