Na Anael
James
Leo usiku
Wayne Rooney anaenda kuweka rekodi mpya pale England itakapovaana na Slovakia
katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018
utakaochezwa majira ya 1:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Rooney anaenda
kuweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyecheza mechi nyingi zaidi kuwahi kutokea
katika Timu ya Taifa ya England kwa kucheza michezo 116.
Kabla ya
mchezo huu wa leo, Rooney anafungana na David Beckham wote wakiwa wamecheza
michezo 115.
Zaidi ya
hapo, Rooney pia anashikilia rekodi ya mfungaji bora wa muda wote kwenye taifa
hilo kwa kufunga mabao 53.
Ikumbukwe
kuwa, hivi karibuni Allan Shearer alinukuliwa akisema ni wakati wa Rooney sasa
kujiengua England na kuwaachia vijana, hali iliyopingwa vikali na Rio Ferdinand
ambaye alisisitiza Rooney aendelee kubaki ili kutoa uzoefu zaidi kwa Vijana.
Hivyo
kuelekea mchezo huo, David Beckham amemimina pongezi kwa nahodha huyo wa
England kwa mafanikio hayo makubwa anayoenda kuyapata.
No comments:
Post a Comment