Na Anael James Waziri_Tall
Ratiba
Jumatano Septemba 7
Simba v Ruvu Shooting
Ndanda FC v Yanga
Tanzania Prisons v Azam FC
Jumatano Septemba 7
Simba v Ruvu Shooting
Ndanda FC v Yanga
Tanzania Prisons v Azam FC
MABINGWA wa
VPL, Ligi Kuu Vodacom, Yanga hii Leo wapo safarini kuelekea Mtwara ili kesho
wacheze Mechi yao ya pili ya Ligi hiyo dhidi ya Ndanda FC.
Yanga wamecheza
Mechi moja tu ya VPL Msimu huu walipoichapa African Lyon na baadae kukamilisha
Ratiba yao ya Makundi ya Mashindano ya CAF.ya Kombe la Shirikisho.
Mechi
nyingine za Jumatano zinahusu Viigogo wengine wa Dar es Salaam, Simba na Azam
FC, wakicheza Mechi zao za 3 kwa Simba kuwepo Jijini Dar es Salaam kucheza na
Ruvu Shooting na Azam FC kuwa Ugenini huko Mbeya kucheza na Tanzania Prisons.
Katika Mechi
zao 2 zilizopita zote Simba na Azam FC zilishinda 1 na kutoka Sare 1.
Kwenye Mechi
hii na Ndanda FC ambao hadi sasa wamecheza Mechi 2 za VPL na kufungwa zote na
Simba na Mtibwa Sugar, Yanga itawakosa Wachezaji wao kadhaa.
Kikosi cha
Yanga cha Wachezaji 20 chini ya Kocha Hans van Pluij kilichosafiri kwa Basi
kwenda Mtwara hakinao Kipa Deogratius Munishi 'Dida' aliefiwa na Baba yake na
Majeruhi Pato Ngonyani, Malimi Busungu na Geofrey Mwashuiya.
Wengine
ambao hawamo Kikosini ni Mapro wao Vincent Bossou aliekuwa na Timu ya Taifa ya
Togo na Haruna Niyonzima aliekuwa na Timu ya Taifa ya Rwanda kushiriki Mechi za
kufuzu Fainali za AFCON 2017 na bado kurejea.
Hata hivyo Kocha Pluijm amesema nia yao ni kushinda Mechi hii na ile ya Jumamosi Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam dhidi ya Majimaji FC.
Nae Kocha wa
Ndanda FC Hamimu Mawazo amesema watapigana ili kuepuka kipigo cha 3 mfululizo
kwenye VPL.
KIKOSI CHA
YANGA KILICHOSAFIRI:
MAKIPA: Ally Mustafa ' Barthez', Beno Kokulanya
MABEKI: Juma Abdul, Hassan Kessy, Mwinyi Haji Mngwali, Oscar Joshua, Mbuyu Twite, Kevin Yondani, Andrew Vincent 'Dante', Nadir Haroub ' Cannavaro'
VIUNGO: Said Juma 'Makapu', Thaban Kamusoko, Simon Msuva, Deus Kaseke, Obrey Chirwa, Yusuf Mhilu
MAFOWADI: Donald Ngoma, Matheo Anthony, Amisi Tambwe
source:Soka in Tanzania
MAKIPA: Ally Mustafa ' Barthez', Beno Kokulanya
MABEKI: Juma Abdul, Hassan Kessy, Mwinyi Haji Mngwali, Oscar Joshua, Mbuyu Twite, Kevin Yondani, Andrew Vincent 'Dante', Nadir Haroub ' Cannavaro'
VIUNGO: Said Juma 'Makapu', Thaban Kamusoko, Simon Msuva, Deus Kaseke, Obrey Chirwa, Yusuf Mhilu
MAFOWADI: Donald Ngoma, Matheo Anthony, Amisi Tambwe
source:Soka in Tanzania
No comments:
Post a Comment